Kilimo cha viazi mviringo - Sehemu ya kwanza (Growing Irish potato - Part one)


MAZINGIRA
Viazi mviringo (Solanum tuberosum) hupendelea maeneo yenye baridi kuanzia 7v°C hadi 26°C kwa siku 75 hadi 135 za ukuaji wake au zaidi, Hali ya joto hupunguza kiasi cha uzalishaji. Zao hili hupendelea udongo tifutifu usiotwamisha maji na wenye rutuba na wenye maozea "Matama huruku" (Organic matter) yenye pH ya 5.0 hadi 5.5.

AINA
Nchini Tanzania kuna mbegu za aina yingi za viazi mviringo ambazo hazalishwa na taasisi mbalimbali za utafiti wa kilimo (Agriculture Research Institute). Kwa upande wa Nyanda za juu kusini mwa Tanzania, Taasisi ya utafiti wa kilimo Uyole (ARI UYOLE) iliyopo mkoani Mbeya inazalisha mbegu za viazi mviringo zifuatazo;

1. Baraka
2. Kikondo
3. Tana
4. Arika

Mbegu zote za hapo juu hufanya vizuri endapo utatunza vizuri kwa kufwata taratibu za kilimo bora.

MAANDALIZI YA MBEGU
Kabla ya kupanda viazi mviringo lazima uwe na mbegu zilizotayari kupandwa. Mbegu zilizo tayari kupandwa huwa na machipukizi au maotea. Kama utapata mbegu zenye maotea unaweza ukazipanda. Pia mbegu hizo au kiazi kimoja cha mbegu kinaweza kutoa mbegu 2 au tatu inategemea ukubwa wa hicho kiazi.

Namna ya kuandaa mbegu kutoka kwenye kiazi kimoja (Viazi vikibwa);
  • Kata kiazi hicho katika vipande kadhaa vyenye maotea kila kimoja, maotea yanaweza yakawa zaid ya moja. Yani kila kipande ulichokata lazima kiwe na maotea (buds).



  • Baada ya kuandaa vipande hivyo vianike juani, au kama jua halipo kwa kipindi cha masika vitandaze mahali pakavu ili vikauke. Lengo la kuanika ni kusaidia zile sehemu zilizokatwa zikauke na zijirudi kama kiazi cha kawaida. Ina maana kwamba ukipanda hivyo hivyo mbegu zitaoza.
Namna ya kuandaa mbegu za viazi visivyo na maotea (Chitting);
  • Chagua viazi mviringo vyenye afya
  • Andaa chumba kisafi chenye giza yani kilichofungwa madirisha na milango ili kuzuia mwanga kupenyeza ndani.
  • Weka turubai au mkeka au masalfeti juu ya sakafu (lengo ni kuzuia unyevu wa sakavu kuozesha viazi)
  • Tandaza viazi kwenye chumba hicho kwa levo au ngazi moja.
  • Funga chumba hicho kwa wiki moja au mbili mpaka utakapoona machipukizi yametoka.
  • Ukiona machipukizi yameota basi viazi vipo tayari kupandwa. (Unaweza ukavikata katika vipande na kuviandaa kama nilivyoeleza hapo juu)




Kuandaa mbegu ni jambo la msingi sana ikiwa ni pamoja na kujua kiasi gani kinahitajika kwa eneo husika (seed rate)

Kwa viazi vikubwa vyenye uzito kuanzia gamu 50 na kuendelea kiasi cha mbegu ni magunia 24 kwa hekta moja.

Kwa viazi vidogo chini ya gramu 50, kiasi cha mbegu ni magunia 8 - 10 kwa hekta moja.

KUPANDA
Viazi mviringo hupandwa kwa nafasi ya sentimita 30 kutoka mche hadi mche na sentimita 40 - 75 kutoka mstari hadi mstari. Pia unaweza kutengeneza matuta kwa kufwata nafasi hizo.

Kama utapanda viazi pasipo kutumia matuta basi hakikisha umelima shamba lako kwa kina cha kutosha cha sentimita 30, na viazi vikishaota rundika udongo maeneo ya shina (earthing) hadi kufikia kina cha sentimita 25.

MATUMIZI YA MBOLEA
Tumia mbolea za asili na mbolea za viwandani. Unaweza ukapandia samadi pamoja na mbolea za viwandani kama DAP. Alafu baada ya mimea kutoa maua, weka mbolea ya CAN halafu endelea kupulizia mbolea za maji kama VIGMAX na nyinginezo. Mbolea ya maji unaweza ukaendelea kupiga kila baada ya wiki moja. Ukifanya hivyo utaona matokeo mazuri ya uzalishaji.


Makala Hii Imehaririwa Mara ya mwisho tarehe: 10/07/2017

Makala na: Lusubilo A. Mwaijengo

1 Comments

Post a Comment

Previous Post Next Post