Namna ya kutengeneza chakula cha kuku wa kisasa (Kuku wa nyama na wa mayai) - Sehemu ya Tatu


SEHEMU YA TATU

MAHITAJI YA CHAKULA KWA KILA HATUA YA UKUAJI
Inampasa mfugaji kuweka kiwango sahihi na sawia kwa kuku wake katika kila hatua ya ukuaji
  • Vifaranga wa kuku wamayai wanahitaji chakula kisichopungua gramu 60 kwa siku. Wskishamaliza kiasi hicho kinachotakiwa wapatie mboga za majani ili kuhakikisha wanakula wakati wote.
  • Kuku wa mayai wanaotaga wanahitaji chakula kiasi cha Gramu 130 hadi 140 kwa siku.
  • Kuku wadogo wa mayai wanaokaribia umri wa kutaga, inatakiwa wapewe chakula kiasi cha Gramu 60 kwa siku kwa muda wa miezi 2 na 1/2 na baadae wapatie chakula cha 'Layer mash' kwa kiwango cha Gramu 140 kwa siku. Pia kwa kuwaongezea lishe zaidi wapatie mboga mboga pamoja na mabaki ya matunda yaliyoliwa.
  • Kuku wa nyama wanahitaji kiasi cha Gramu 67 kwa siku (Kwa aina zote za chakula yaani 'Broiler starter' na 'Broiler finisher') mpaka siku watakapofikia umri wa kuchinjwa (Siku 35 - 42)

ILANI:
Kuku wa aina zote (wa mayai au wa nyama) wanaathiriwa sana na sumu kuvu itokanayo na chakula (aflatoxins). Sumu kuvu hii hutokana na malighafi za chakula zilizooza kama mahindi wakati wa kutengeneza chakula. Epuka kutumia mahindi yaliyooza wakati wa utengenezaji wa chakula cha kuku.


NI WAPI UTANUNUA MALIGHAFI ZA KUTENGENEZEA CHAKULA CHA KUKU?
Mfugaji anaweza kununua malighafi za kutengenezea vyakula hivi kama nafaka mbalimbali, Pumba, unga wa samaki n.k kwa kuvipata maeneo ya sokoni. Masoko mbalimbali makubwa nchini Tanzania huuza malighafi haya. Pia kupata aina mbalimbali za pumba hupatikana kwenye mashine mbali mbali ya kukoboa au kukamua mafuta ya alizeti kama unahitaji mashudu ya pamba au ya alizeti.

Kwa mahitaji ya vionjo (additives) kama 'Pre-mixes', 'Amino acids', Unga wa mifupa, chokaa n.k ambavyo ndio nyongeza ya virutubisho mbalimbali na muhimu kwenye chakula cha kuku hupatika kwenye maduka ya kuuza pembejeo za mifugo yanayopatikana maeneo mbalimbali nchini Tanzania.


MAMBO MUHIMU NA YA KUZINGATIA WAKATI WA UTENGENEZAJI CHAKULA CHA KUKU
Wakati wa kutengeneza chakula cha kuku ni muhimu kufanya majaribio kwa kuwatenga baadhi ya kuku wachache. Kuku hao uliowatenga walishe chakula hicho kwa muda fulani ili kuona matokeo ya ubora wa chalula chako. Kama chakula chako ni kizuri kuku wa nyama watakua kwa kasi na kuku wa mayai wataongeza uzalishaji wa mayai kwa ongezeko lisilopungua yai moja kila baada ya masaa 27.

Nunua Samaki au Unga wa samaki uliosagwa kutoka kwa wauzaji wanaozingatia ubora. Kama umepanga kutumia unga wa samaki kwa kutengenezea chakula hakikisha una ubora wa kutosha, kwani inaweza ikatokea ukanunua samaki au unga wa samaki uliochafuliwa au kuvunda. Unga wa samaki uliochafuliwa ni hatari kwa afya ya kuku, Mfugaji anashauriwa kutumia Unga wa soya kama atashindwa kupata Samaki au Unga wa samaki wenye ubora.

Kabla ya kuchanganya malighafi za chakula cha kuku, changanya kwanza vionjo (additives) kama Amino acids, Premix, n.k. ndipo umalizie kuchanganya malighafi zingine kama Mahindi, pumba za mahindi, Unga wa samaki n.k.

Wakati kuchanganya chakula cha kuku, tumia madumu maalumu ya kuchanganyia kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini. Chonde chonde usitumie koleo au sepetu kuchanganya chakula cha kuku kwa sababu malighafi hazitachanganyika vizuri.






Kama una swali, ushauri au maoni yoyote kuhusiana na makala hii, usisite kuyaandika hapo chini. Karibu sana!. Tukutane tena kwenye makala zijazo, Nakutakia siku njema.

<<< SEHEMU YA PILI

*MWISHO WA MAKALA HII*

Kama una maoni au ushauri wowote kuhusiana na makala hii usisite kuacha maelezo yako hapo chini, Karibu sana!.

Makala na: Lusubilo A. Mwaijengo

4 Comments

  1. Ahsanteni sana pia unafanyaje au jinsi gani utaweka chakula mpak ujue kuku kala gram kadhaa

    ReplyDelete
  2. tunaomba tupate maelezo ya kutosha kuusu kuchanganya na jinsi ya kuakikisha uyo kuku kala ujazo unaostaili

    ReplyDelete
  3. MNAHUSIKA NA UUZAJI WA MALIGHAFI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA KUKU?NA MNAPATIKANA WAPI?

    ReplyDelete
    Replies
    1. umetajiwa malighafi tafuta kulingana na eneo ulipo....

      Hatimae utakuja uliza unafanyafanyaje mpka kuku ale...

      Delete

Post a Comment

Previous Post Next Post