Zifahamu faida za kunywa maji ya vuguvugu


Habari ndugu wasomaji wangu? Leo nimekuja na maada muhimu ya Afya kuhusiana na umuhimu wa kunywa maji ya vuguvugu kila asubuhi mara tu unapoamka. Baadhi ya watu miongoni mwenu wamekua wakitumia maji ya vuguvugu kama dawa ya kudhibiti magonjwa mbalimbali waliyonayo.

Watafiti wa mambo ya Afya wamethibitisha kwamba maji ya vuguvugu yanatibu magonjwa mbalimbali kwa asilimia 100% na kuufanya mfumo wa mwili ufanye kazi vizuri. Magonjwa hayo ni kama ifuatavyo;
  • Kipanda uso (Migraine)
  • Presha ya kupanda
  • Presha ya kushuka
  • Maumivu ya viungo
  • Mapigo ya moyo yanayoongezeka na kupungua kwa kasi
  • Kifafa (Epilepsy)
  • Kuongezeka kwa kiwango cha mafuta mwilini (Cholesterol)
  • Kikohozi
  • Uchovu wa mwili
  • Maumivu ya magoti
  • Athima
  • Itilafu ya mishipa ya damu
  • Magonjwa yanayohusiana Mfuko wa kizazi na mfumo wa mkojo wa mwanamke.
  • Kuongeza hamu ya kufanya tendo la ndoa pamoja na nguvu za kiume
  • Matatizo ya tumbo kama vidonda vya tumbo n.k
  • Kukosa hamu ya kula.
  • Magonjwa yote yanayohusiana na macho, masikio pamoja na koo.
  • Maumivu ya kichwa
  • Na magonjwa mengine mengi....

*MUHIMU
Ukiugua nenda hospitali kwa uchunguzi na matibabu zaidi. Matumizi haya ya maji ya vuguvugu si kwa wagonjwa tu bali hata wasiougua, inasaidia kuimarisha afya yako katika kiwango bora zaidi.

NAMNA YA KUTUMIA MAJI YA VUGUVUGU
Fwata kanuni zifuatazo kutumia maji ya vuguvugu
(a) Mara tu unapoamka kunywa maji ya vuguvugu glasi au vikombe viwili kabla ya kula chochote. Mwanzoni utapata taabu sana kumaliza vikombe hivyo viwili vya maji lakini siku zinavyozidikwenda utaendelea kuzoea taratibu hatimae utaweza kabisa.

(b) Ili kupata matokeo mazuri ya afya yako, kunywa maji ya vuguvugu kila siku kadri utakavyoweza, iwe ni sehemu ya maisha yako. Utashangaa kuona mabadiliko makubwa kwenye mwili wako.

*MUHIMU
Baada ya kunywa maji hayo, kula chochote baada ya dakika 45.

MAJI YA BARIDI NI HATARI KWA AFYA YAKO!!
Kama hujaona madhara ya maji ya baridi katika umri mdogo basi utaona madhara yake baadae ukifikia utu uzima/Uzee.


Madhara ya kunywa maji ya baridi;
  • Husabisha mishipa ya moyo (Veins) kuziba na kusabisha mshituko wa moyo (Heart attack), tatizo hili husababisha watu wengi kufariki ghafra.
  • Pia husababisha matatizo kwenye Ini. Watu wengi wanaosubiri kupandikizwa Ini baada ya kuharibika ni wahanga wa kunywa maji ya baridi.
  • Huathiri ukuta wa ndani wa tumbo
  • Huathiri utumbo mkubwa na kusababisha Kansa.
*Kama una maoni au ushauri kuhusu makala hii, tuandikie hapo chini; Karibu!.

Makala na: Lusubilo A. Mwaijengo

Post a Comment

أحدث أقدم