Ufugaji wa kuku wa Mayai - Sehemu ya Kwanza (Layer Poultry Farming - Part One)


SEHEMU YA KWANZA

Ufugaji wa kuku wa mayai ni ufugaji wa kuku wa kisasa wanaotaga mayai tu, mayai hayo ni kwa ajili ya kuliwa tu sio kuanguliwa, kwa sababu hayajarutubushwa (Not-fertile) na dume (Jogoo). Kuku hawa wa mayai ni aina pekee ya kuku ambao wanahitaji kulelewa kwanzia wakiwa vifaranga hadi wakiwa wakubwa. Kuku hawa wanaanza kutaga mayai wakiwa na umri wa wiki 18 hadi 19 (Miezi 41/2 hadi 5), Wataendelea kutaga mayai mfululizo mpaka watakapofikia umri wa wiki 72 hadi 78 (Miezi 18 hdi 20). Kama unataka kuzalisha vifaranga kwa ajili ya kupata kuku wa mayai, hakikisha unaangalia tabia za kuku jike na jogoo kabla ya kuwakutanisha ili kupata mayai ya vifaranga. Kuna aina mbalimbali za jamii za kuku wanaozalisha sana mayai, na wanapatikana Duniani kote.

AINA ZA KUKU WA MAYAI (LAYER BREEDS)
Kuku wa mayai wamegawanyika katika makundi makubwa mawili kulingana na rangi ya mayai. Ufuatao ni mchanganuo wa makundi haya mawili;

1. Kuku wanaotaga mayai meupe (White Egg laying Hens)
Hawa ni aina ya kuku wa mayai wenye maumbile madogo, na wanakula chakula kidogo pia wataga mayai madogo na yenye gamba jeupe. Zifuatazo ni aina mbalimbali za kuku hawa ambao hufugwa sana na watu wengi;

  • Isa White
Photo Credit: www.isa-poultry.com
  • Lehman White / Lohmann White
Photo Credit: www.hylinena.com
  • Nikchik
Photo Credit: www.hn-int.com
  • Bab Cock BV-300
Photo Credit: www.babcock-poultry.com
  • Havard White
  • Hi Sex White
Photo Credit: www.hisex.com
  • Sever White
  • Hi line / Hyline White



Photo Credit: www.hyline.com
  • Bovanch White
Photo Credit: www.bovans.com

2. Kuku wanaotaga mayai ya Kahawia (Brown Egg Laying Hens)
Hawa ni kuku wa mayai wenye maumbile makubwa, na wanakula chakula kingi zaidi ukiringanisha na kuku wanaotaga mayai meupe. Wanataga mayai makubwa kuzidi kuku wengine wa mayai, Pia mayai yao yanakua na gamba lenye rangi ya kahawia (Brown)
Zifuatazo ni aina mbalimbali za kuku hawa ambao hufugwa sana na watu wengi;

  • Isa Brown
Photo Credit: www.backyardchickencoops.com.au
  • Hi Sex Brown
Photo Credit: www.hisex.com
  • Sever 579
  • Lehman Brown / Lohmann Brown

Photo Credit: www.hylinena.com
  • Hi Line Brown

Photo Credit: www.hyline.com
  • Bab Cock BV-380
Photo Credit: www.babcock-poultry.com
  • Gold Line / Bovans Goldline

Photo Credit: www.poultrykeeper.com
  • Bablona Tetro
  • Bablona Harko
  • Havard Brown n.k.
KUCHAGUA AINA YA KUKU WA MAYAI (LAYER HEN SELECTION)
Kabla ya kuchagua aina ya kuku unaotaka kufuga, hakikisha unakua na taarifa muhimu kuhusiana na tabia za hao kuku ikiwemo kiwango kikubwa cha kutaga mayai. Zifuatazo ni tabia za kuku wanaofaa katika uzalishaji wa mayai;
  • Kwa ufugaji wa kuku wa mayai kibiashara, hakikisha unachagua aina kuku wanaotaga kiwango kikubwa cha mayai.
  • Nunua vifaranga wenye afya njema, wanaotoka kwenye wazalishaji wenye uwezo na wanaozingatia taratibu zote za Uangulishaji bora.

KULEA VIFARANGA (KEEPING CHICKS)
Kabla ya kuwaleta vifaranga nyumbani kwako hakikisha unafanya maandalizi yafuatayo;
  • Hakikisha umeandaa sehemu maalumu ya kuwalea vifaranga (Brooder)
  • Hakikisha una taa za kandili au balbu zinazotumia umeme au jiko la mkaa kwa ajili ya kuwapatia joto vifaranga.
  • Hakikisha umeandaa matandazo ya kuweka kwenye sakafu kama maranda ya mbao,mapumba ya mpunga n.k. kwa ajili ya kuwapa joto
  • Eneo la mita mraba 1 (1m2) hutosha vifaranga 20 hadi kufikia umri wa wiki 4
  • Dhibiti joto bandani au sehemu maalum ya kuwalea vifaranga (Brooder) hadi kufikia nyuzijoto 35°C kwa vifaranga wa siku moja na nyuzi joto 24 - 27°C kwa vifaranga wenye umri wa wiki 1.
Kufahamu kama joto uliloweka linawafaa vifaranga wako au lah, chunguza hali ifuatayo;

*Ukiona vifaranga wamekusanyika pamoja kwa kuzunguka chanzo cha joto ina maana kwamba kuna kiasi kidogo sana cha joto.

*Ukiona vifaranga wamekaa mbali na chanzo cha joto, ina maana kuna kiwango kikubwa cha joto.

*Ukiona vifaranga wametawanyika sehemu zote, ina maana kwamba joto lililopo linawafaa.

Punguza kiwango cha joto kadiri vifaranga wanavyoendelea kukua.

MUHIMU
Wiki ya kwanza baada ya kuanguliwa, vifaranga wengi huwa hawataki kunywa maji hii ni kwasababu ya hekaheka za kuwasafirisha kutoka sehemu moja hadi nyingine. Kwa hiyo inatakiwa uweke maji ya kutosha kwenye eneo lao lililotengwa (Brooder), pia inatakiwa uwafundishe kunywa maji. Changanya maji yao ya kunywa na Glukosi (5% Glucose) ili wapate nguvu haraka. Pia Wapatie aina yoyote ya Multivitamin na uchanganye na maji yao ya kunywa, Multivitamin hii husaidia sana kuku pale wanaposafirishwa umbali mrefu, hupunguza Uchovu wa vifaranga na upungufu wa maji na pia husaidia kuwafanya vifaranga warudi kwenye hali yao ya kawaida.


Makala na: Lusubilo A. Mwaijengo

4 تعليقات

  1. Ntawezaje kupunguza joto kwenye banda wakati natumia bulb ua umeme?

    ردحذف
  2. Naomba msaada jmn mm nataka kuanza kufuga kuku wa mayai kuku miambili je? Niandae kiasi gan

    ردحذف
  3. Naitaji kuanza kufuga kuku mambo gani muhim yakuzingatia kuku wa mayai

    ردحذف

إرسال تعليق

أحدث أقدم